WACHEZAJI YANGA WAGOMEA MAZOEZI, ZAHERA ATAMKA JAMBO
Wachezaji wote wa Yanga unaowajua wewe ambao usajili wao upo CAF jana Ijumaa waligoma kufanya mazoezi huku Kocha Mwinyi Zahera akiwasihi viongozi wawaambie mashabiki wa timu hiyo ukweli.
Zahera alifika mazoezini kwenye Uwanja wa Polisi Kurasini asubuhi akajikuta yupo na wachezaji watano tena wote ni wageni wengine hata mashabiki wa Yanga hawawajui.
Wachezaji wote waliocheza mechi ya Gor Mahia hakuna hata mmoja aliyeonekana mazoezini na Zahera hakuwa na taarifa yoyote lakini Championi limejiridhisha kwamba wameambizana kugoma kufanya mazoezi wakishinikiza walipwe mishahara yao ya miezi mitatu na kushinikiza pia mashabiki wajitokeze kuokoa jahazi.
Yanga Jumatano ya wiki hii ilipigwa mabao 4-0 na Gormahia kwenye mechi ya Shirikisho na timu hizo zitarudiana Dar es Salaam Ijumaa ijayo saa 1.00 usiku.
duuuuh hii ni aibuu kubwaa ila mjinga
ReplyDeleteMiezi mitatu hawajalipwa.ndiyo maana walicheza chini ya kiwango Nairobi na kuishia kichapo cha mbwa mwizi!Yanga watapata tabu sana.Poleni
ReplyDeleteShidaĆ aa
ReplyDeleteHivi zamani si kulikuwa na watu wanatekaga timu ikifanya vibaya siku hizi hawapo
ReplyDeleteNi ninyi waandishi Wa habari ndio mnaoua timu zetu.Kwa kushindwa kuleta habari making za kiuchunguzi maoema.Shuda ya Yanga haina uongoxi.ni wapiga dili tu
ReplyDeleteKwa bipj unsondoa,Yanga tatizo ni uonhkxi haina.waliopo ni wapiga dili tu.( utaiondoa na hii)
ReplyDeleteHaya Ni mapito tu.hat kwa mtani yakuwakuta Lin yamepita.muhimu mshikamano.ytapita tu..Yanga daima mbele..
ReplyDeleteWatapata taabu Sana
ReplyDeleteYanga wauze timu wafuge kuku.
ReplyDeleteTuwaombee wenzetu kwa sala wakati wao huu mgumu upite kwa heri pasipo kupandisha jazba busara itumike kupunguza hasira na kuleta matumaini ya kuwepo kwa amani ndani ya klabu.
ReplyDeleteViongozi wa Yanga waache kukomaaa waeleze ukweli ikiwezekana wawape wawekezaji timu ili mambo yakawe sawa vinginevyo ni aibu tuupu.... Tunakoelekea nikushuka daraja kabisa
ReplyDelete