August 20, 2018


Basi la Kampuni ya Saratoga lililokuwa likitoka Kigoma kuelekea Sumbawanga limewaka moto na kuteketea katika Kijiji cha Kazuramimba mkoani Kigoma huku chanzo cha moto huo kikiwa hakijajulikana bado. 

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, ACP Martin Ottieno amesema jeshi lake linachunguza chanzo cha moto huo. 

Bado haijafahamika iwapo kuna vifo au majeruhi kutokana na ajali hiyo mbaya.

Eneo la tukio, baada ya basi mali la Saratoga lililokuwa likitoka mkoani Kigoma kwenda Sumbawanga kuteketeka kwa moto katika Kijiji cha Kazuramimba mkoani Kigoma. 

Abiria wote 60 waliokuwa ndani ya basi hilo wamepona na baadhi ya mizigo imeokolewa.

Endelea kufuatilia mtandao wetu kwa taarifa zaidi hapo baadaye.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic