September 18, 2018


Baada ya kukishuhudia kikosi chake mbashara kikicheza dhidi ya Stand United, Kocha wa Yanga, Mkongomani, Mwinyi Zahera, juzi aliweka rekodi ya kukaa kwa mara ya kwanza kwenye benchi la ufundi.

Kocha huyo ambaye alikuwa hana kibali cha kazi kwa muda mrefu, alikuwa sehemu ya benchi la ufundi katika Uwanja wa Taifa ikiwa ni mara ya kwanza tangu awasili nchini.

Zahera alianza kukaa kwenye benchi hilo wakati Yanga ikicheza mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda, mechi ambayo walifungwa bao 1-0.

Mkongomani huyo ameweka rekodi hiyo tangu kuondoka kwa aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga, George Lwandamina aliyeondoka bila kuaga kutokana na kutofikiana mwafaka kwa baadhi ya mambo na mabosi wake wa zamani.

Wakati huo kikosi cha Yanga kitaendelea na maandalizi ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Coastal Union utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa Jumatano ya wiki hii.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic