September 2, 2018


Kikosi cha Simba kimeendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Gymkana uliopo jijini Dar es Salaam tayari kwa mechi za Ligi Kuu Bara.

Kikosi hicho kimeongezeka baada ya wachezaji waliokuwa wamechelewa kujiunga na kambi ya Taifa Stars kisha kuondolewa, wameanza mazoezi na wenzao tayari kukabiliana na Ndanda huko Mtwara.

Ndanda itaikaribisha Simba kwenye Uwanja wao wa Nangwanda Sijaona Septemba 15 2018.

Wakati Simba wakijiandaa, Ndanda FC nao wako katika maandalizi moto wakijiandaa kujibu mapigo ya mnyama ambaye amedhamiria kuuchukua ubingwa wa ligi kwa miaka mitano mfululizo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic