October 4, 2018


Kwa sasa hatua tuliyofikia angalau kidogo tunaweza tukapongeza jinsi ambavyo ush­indani ulivyo kwenye Ligi Kuu Bara. Bado ligi ni mbichi na hakuna ambaye amelalamika kuhusu matendo ya kununua matokeo wala kuonewa.

Ni jambo ambalo linaleta neema na kuweza kuanza kukubalika kwa baadhi ya watu ambao wanafuatilia soka kwa kuwa hilo la ushindani kwa sasa lipo wazi ligi ni ngu­mu kabisa kila timu inakomaa kuhakikisha inafikia malengo yake.

Habari ambayo imekuwa kubwa ni kutokana na mchezo wa Simba na Yanga ambao uli­chezwa wikeendi iliyopita ka­tika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Nimeufuatilia kwa ukaribu mchezo ule na nimegundua mengi ya ajabu na kushanga­za kwenye soka letu.
Jambo kubwa ambalo bado lisipotazamwa kwa ukaribu linaweza kuleta hatari wakati mwingine ni utaratibu ambao unakuwa kwenye mageti ya kuingilia, yaani hauvutii hata kidogo hasa kwa mechi kama ya Simba na Yanga.

Ubabe wa askari wetu bado upo palepale hata uwe na kitambulisho au tiketi wala hawakuelewi, sijajua wana­taka kuendesha mechi hizi kwa mfumo upi jambo ambalo linaweza kuwa sawa kwa wote ambao wanafika Uwanja wa Taifa kutazama mechi hiyo.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linapaswa kulitazama hili kwa jicho la kipekee kwa sababu mashabiki huwa wa­nakosa raha kabisa wakati wa kuzishuhudia timu zao wazipendazo, sijajua kwa nini mchezo wa mpira ambao una amani unatawaliwa na shari.

Nimebahatika kuwao­na namna askari walivy­okuwa wakiwapiga baadhi ya mashabiki wakidai wal­ishindwa kufuata utaratibu hasa kwenye geti kubwa la kuingilia, hili nalo halipo sawa, kuna namna nzuri ya kuweza kuwaelekeza mashabiki na wakaelewa.

Baada ya mchezo huo, tu­meona timu yetu ya taifa, Taifa Stars imeingia kambini ikijiandaa na mchezo ujao wa kufuzu kwa Fainali za Kombe la Mataifa Afrika (Afcon) dhidi ya Cape Verde.

Rai yangu ni kwamba wache­zaji mnapaswa kutimiza wajibu wenu ipasavyo kwa kuonyesha juhudi isiyo ya kawaida hasa katika kuipeperusha Bendera ya Taifa huko kimataifa.

Muda pekee wa kuweza ku­hakikisha kwamba kila kitu katika soka kinawezekana hasa kwa kufanya kweli ka­tika mashindano hayo ni sasa kwa kuwa tuna wachezaji wengi ambao wana uzoefu na mashindano ya kimataifa.

Jambo kubwa la muhimu ambalo mnapaswa kufan­ya ni kuhakikisha kwamba mnaaonyesha nidhamu ya hali ya juu ndani na nje ya uwanja hali ambayo itasaidia kupata matokeo mazuri katika mich­ezo ambayo mtashiriki.

Kuna tabia ambayo wache­zaji wengi huwa nayo hasa baada ya kuitwa timu ya tai­fa, wanadhani kwamba wao wanaweza kufanya kila kitu jambo ambalo linawafanya wanavimba kabla hata ya kucheza mpira.

Kuvimba ama kuwa na dharau ni kosa kubwa kwa mchezaji kwani kwa kufanya hivyo kunadidimiza ule uwezo ambao unao na hata ukipewa nafasi utashindwa kuitumia vema.

Yatupasa tubadilike na tu­badilishe makosa ambayo tu­liyafanya wakati tunacheza na timu ya Uganda, hivyo kupata ushindi iwe ndio dhamira yetu kuu ya kwanza katika mchezo wetu huo ujao.

Mara nyingi nimekuwa ni­kiwaambia wachezaji ambao napata bahati ya kuonanana nao ni kwamba kuitwa timu ya taifa ni nafasi ambayo wamei­pata adimu sana na ni kubwa kuliko vile ambavyo wanafiki­ria, hivyo wanapaswa wafanye makubwa zaidi.

Kwa kufanya hivyo kutasaid­ia kuongeza thamani ya mche­zaji maradufu hali itakayoanza kufungua milango ya mafani­kio taratibu bila papara yoyote ile katika ushindani ambao tupo kwa sasa.

Niseme tu kwamba kwa hatua ambayo kwa sasa tu­mefikia sio mbaya kwani kuna kitu ambacho kinaonekana kwa wachezaji na wanaweza kufanya maajabu hasa katika mashindano ya kimataifa am­bayo tunashiriki.

1 COMMENTS:

  1. Inawezekana meseji ikawa sent au ujumbe umefika. Ila vyama vingi vya mpira au taasisi zinazoshughulikia Timu za Taifa Africa zimeingia migogoro na wachezaji wanaokwenda kutumikia timu zao za taifa. Suala la uzalendo sawa lakini lazima tuwe wawazi juu ya maslahi ya wachezaji hao wa timu ya Taifa wakati wanapokwenda kutumikia taifa lao kama Tanzania basi lazima tuwe wawazi juu ya suala hili kungali mapema ili kuepusha uwezekano wa kuja kuingia katika migogoro isio ya lazima kati ya wachezaji na mamlaka husika. Tunaimani FIFA au CAF lazima watakuwa na fungu fulani kuhusiana na mashindano husika basi chonde kwenye fungu hilo wachezaji ndio wawe wanufaika wa kwanza na lazima kuwe na uwazi. Mpira sasa unahitaji motisha kwa wachezaji kwani ushindani ni mkubwa hata wa huo wa motisha kwa wachezaji wa timu nyengine kwa hivyo ni vizuri kusoma alama za nyakati .

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic