Azam FC walianza kumtambulisha mshambuliaji Obrey Chirwa na kumpa kandarasi ya mwaka mmoja akiwa ni mchezaji huru kutoka timu ya Nogoom ya Misri.
KMC walifuata kwa kumpa kandarasi ya mwaka mmoja Elias Maguli wakamtambulisha mchezaji kutoka Singida United Salum Chuku ambaye ni beki wa kushoto kwa kandarasi ya mwaka mmoja.
Wachezaji wengine ambao wameshasajiliwa kwenye dirisha dogo ni pamoja na Miraji Adam kutoka Singida United amesajiliwa Coastal Union, Dauda Bortu amesajiliwa na Singida United kutoka Liberia.
Alliance FC ya Mwanza wamempa kandarasi ya miaka miwili kocha Malale Hamsini kutoka Ndanda FC kuziba nafasi ya Mbwana Makata aliyejiuzulu kwa madai ya kuingiliwa mamlaka na Mkurugenzi wa kituo hicho James Bwire.
0 COMMENTS:
Post a Comment