November 26, 2018


Beki wa kulia wa Sim­ba, Shomari Kapombe, amefanyiwa upasuaji wa mguu kufuatia kuu­mia enka kwenye kambi yaT­aifa Stars nchini Afrika Kusini.

Beki huyo alikuwa kwenye kambi ya timu hiyo iliyokuwa ina­jiandaa na mchezo wa kuwania kufuzu Afcon dhidi ya Lesotho katika mchezo uliopigwa nchini Lesotho, wikiendi iliopita.

Beki huyo ambaye alilazimika kubakia nchini humo kwa ajili ya kupatiwa matibabu, juzi alifanyi­wa upasuaji wa mguu wake katika hospitali moja kubwa kwenye Jiji la Pretoria, Afrika Kusini.

Lwa mujibu wa Championi Jumatatu, mwenyekiti wa timu hiyo, Swedy Mkwabi alisema up­asuaji huo utamlazimu Kapombe kukaa nje ya uwanja kwa wiki sita.

“Kesho Jumatatu (leo) atak­wenda tena hospitali kuonana na daktari wake ili kuangalia maen­deleo baada ya upasuaji kwa sababu atakuwa nje kwa muda wa wiki sita isipokuwa atarejea nchini wakati wowote kulingana na dak­tari wake atakavyokuwa ameon­gea naye,” alisema Mkwabi.

CHANZO: CHAMPIONI

2 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic