November 27, 2018


Baada ya juzi Ju­mamosi Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutangaza majina ya waliopit­ishwa kuwania nafasi mbalim­bali za uongozi wa Yanga, huku ikisisitiza kutomtambua Yusuf Manji kama mwenyekiti wa klabu hiyo, aliyekuwa kati­bu mkuu wa timu hiyo, Charles Boniface Mkwasa ameibuka na kutoa neno.

Mkwasa ambaye hivi karibuni aliachana na nafasi yake ya uka­tibu mkuu wa Yanga ili akatibiwe tatizo la moyo lililokuwa likim­sumbua kwa muda mrefu, ameli­ambia Championi Jumatatu kuwa TFF isiuchukulie poa mgogoro uliopo sasa kati yake na Yanga kuhusiana na Manji.

Mkwasa alisema licha ya kuwepo kwa upungufu mbalimbali wa kikatiba juu ya suala hilo, TFF inapaswa kutumia busara ili kuhak­ikisha Yanga inakuwa sawa na siyo kusababisha mvu­rugano.

“Kama Manji amekubali kurudi katika nafasi yake ya uongozi kutokana na uamu­zi wa wanachama wa Yanga walioutoa kwenye mkutano mkuu wa klabu uliofanyika mwezi Juni, mwaka huu, TFF inapaswa kukubaliana na maamuzi hayo kwani hata katiba ya klabu inase­ma kuwa wenye maamuzi ya mwisho juu ya jambo lol­ote lile ni wanachama kupi­tia mkutano mkuu.

“Nakumbuka katika mku­tano huo, mimi ndiye ni­likuwa katibu ambapo wanachama kwa pamoja waliikataa barua ya kujiu­zulu ya Manji na wakanitaka niwaandike barua ya kutaar­ifu kuhusiana na uamuzi wao huo, nilifanya hivyo na barua nyingine nikaipeleka TFF na katika mamlaka ny­ingine.

“Baada ya TFF kui­pokea barua hiyo ilibidi wamwondoe aliyekuwa Kai­mu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga katika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, kutokana na maamuzi ya mkutano mkuu wa klabu yaliyofanywa na wanach­ama ya kugomea barua ya kujiuzulu kwa Manji, kwa hiyo hana sifa za kuwa ka­tika nafasi hiyo kwa sababu Manji bado ni mwenyekiti Yanga.

“Kwa hiyo kutokana na hali hiyo, TFF inapaswa kutumia busara kulimaliza tatizo hilo kwa faida ya soka la Tanzania hata kama kuna upungufu wa kikatiba am­bao haukufuatwa ambao wao ndio wanasimamia la­kini mwisho wa siku wenye maamuzi na Yanga ni Yanga wenyewe, tena kupitia mku­tano wao mkuu,” alisema Mkwasa ambaye kwa sasa hafanyi kazi yoyote kuto­kana na ushauri aliopewa na madaktari wake waliokuwa wakimtibu tatizo la moyo li­lilokuwa likimsumbua.

CHANZO: CHAMPIONI

3 COMMENTS:

  1. Mkwasa tulia uuguze moyo wako, usitafute balaa, Manji sio bubu ila tunamgeuza Mungu

    ReplyDelete
  2. Mi naungana na wanachama, wapenzi na washabiki wanaotaka uchaguzi ufanyike. Timu imeendeshwa kiholela kwa muda mrefu sasa. Sidhani kama kuna mantiki ya kutofanya uchaguzi. Kama Manji anataka kuendelea anatakiwa atoke na kutoa kauli yake mbele ya wanachama na washabiki wote na hata Taasisi inayosimamia michezo nchini. Wachezaji wamekosa morali kwa kuwa hawajui kuhusu kesho. Endapo kama mishahara na mazingira mengine ya kazi yangekuwa yanaendelea vizuri tungesema ngoja tuvumilie.

    Tufanye uchaguzi na tuache propaganda za mpira zipite. Wasiotaka maendeleo bado wataendelea kumkumbatia Manji kama mwenyekiti. Upande wangu naona kabisa kama Manji anataka kurudi arudi kuwa mwekezaji na si mwenyekiti tena

    ReplyDelete
    Replies
    1. 1. Kabla ya uchaguzi huo mmejiandaaje ukigeuka kuwa uchafuzi badala ya uchaguzi?
      2. Wakati huu wa kipindi cha mpito na dirisha la usajili likiwa wazi mnaisaidiaje klabu yenu?
      3. Je TFF ilipomuondoa Sanga ilimaanisha nini? Mamlaka nyingine kwanini zilikaa kimya wakati wote huo? Je ni maslahi ya nani Yanga kukiwa na mgogoro?

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic