March 2, 2019


WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba, wanatarajia kuon­doka Jumanne ijayo kwenda Algeria kupambana na JS Saoura katika mwendelezo wa michuano hiyo ambayo kwa sasa ipo hatua ya makundi.

Katika mchezo huo ambao unatara­jiwa kuchezwa Machi 9, mwaka huu nchini Algeria, Simba itashuka uwanja­ni ikiwa na kumbukumbu ya kuitandika timu hiyo mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza uliochezwa jijini Dar.

Mratibu wa Simba, Abbas Ally ameliambia Championi Ijumaa kuwa: “Maandalizi kwa ajili ya safari yetu ya Algeria yanaendelea vizuri na kama mambo yatakaa sawa basi Jumanne ijayo tutaondoka kwenda huko.

“Hata hivyo, kwa sasa sijawa na uhakika kwa asilimia mia moja kwa sababu bado tunaendelea na utaratibu wa safari hiyo lakini kwa harakaharaka inaweza ikawa siku hiyo.”

Simba inahitaji ushindi katika mch­ezo huo ili ijitengenezea mazingira mazuri ya kutinga robo fainali.

Kwa sasa Simba inashika nafasi ya pili katika Kundi D ikiwa na pointi sita wakati Al Ahly ya Misri inaongoza ikiwa na pointi saba. JS Saoura wana pointi tano nafasi ya tatu, huku AS Vita ya DR Congo inaburuza mkia hilo ikiwa na pointi nne.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic