UONGOZI wa timu ya Brighton umemfukuza kazi Meneja wa kikosi hicho Chris Hughton baada ya kuiongoza timu yake kumaliza ikiwa nafasi ya 17 kwenye Ligi Kuu England.
Hughton ameshinda michezo mitatu pekee kati ya 23 ya mwisho ya ligi ambayo aliyosimamia.
Mwenyekiti wa timu hiyo, Tony Bloom amesema kocha huyo ameiweka thamani ya timu hiyo kwenye hali ya hatari.
Mkataba wa Hughton mwenye miaka 60, ulikuwa unatarajiwa kumalizika mwaka 2021 nafasi yake inatajwa kuchukuliwa na Graham Potter, 43..
0 COMMENTS:
Post a Comment