May 3, 2019

WINGA wa kikosi cha Yanga, Mrisho Ngassa amesema kuwa anahitaji kuitumikia timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kwa kuwa bado ana uwezo na nguvu kulitumikia Taifa.

Ngassa amekuwa msaada ndani ya Yanga kwa kutimiza majukumu yake ipasavyo kwani alihusika kuipa pointi tatu muhimu kwenye mchezo wao wa ligi dhidi ya Azam kwa kufunga bao lililodumu mpaka dakika ya 90.

"Bado nina nguvu na uwezo wa kuitumikia timu yangu ya Taifa hivyo nikiitwa ni lazima nionyeshe uwezo zaidi, kikubwa ambacho kinanifanya niamini ninaweza kuitwa ni rekodi yangu ya kucheka na nyavu kuwa wazi, ni suala la muda tu," amesema Ngassa.

Yanga imejikita kileleni ikiwa na ponti 80 baada ya kucheza michezo 34 ya ligi imebakiwa na michezo minne mkononi kwa sasa.




2 COMMENTS:

  1. Kwakuifungia yanga Goli moja ndio achukuliwe kikosi cha timu ya taifa?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic