May 21, 2019


Baada ya kuwa na asilimia 100 za kuukosa ubingwa wa Ligi kuu msimu huu, Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema kuwa ni lazima wabebe ndoo hiyo msimu ujao.

Licha ya kumaliza katika nafasi ya pili, Zahera amesema timu yake imefanikiwa sana msimu huu kulingana na mazingira waliyokuwa nayo mwanzo wa ligi.

Pia amedai akiwa msimu wake wa kwanza Tanzania ameifahamu vizuri ligi kuu ya Tanzania aina ya wachezaji wanaohitajika na mbinu za kutumia msimu ujao.

"Tulianza kwa kuwa na malengo ya kumaliza nafasi ya sita au saba, lakini baada ya kuona tunafanya vizuri licha ya kuwa na changamoto nyingi, tukasema tujaribu kuwania ubingwa,"

"Bado naamini tulistahili kushinda kombe kama siyo kudhurumiwa baadhi ya michezo na marefa na TFF.

Sasa nafurahi timu imepata viongozi wapya nimewaambia wajipange kwa ajili ya msimu ujao"

"Hatutaki tena haya ya mwaka huu yatukute msimu ujao. Tunahitaji kuwa na timu imara itakayoshinda na kutwaa ubingwa mapema.

"Tutatengeneza timu imara, tutasajili wachezaji wa kiwango cha juu ambao watafanya timu yetu iwe kali".

3 COMMENTS:

  1. Ikiwa mmedhulumiwa una haki kuudai ubingwa wako. Na hiyo msimu unsokuja Pia usahau

    ReplyDelete
  2. Uongozi mpya yaani umekuja na nuksi....wale Wanayanga wenye hasira wako wapi? Habari zinaendelea kuwa si nzuri sana wachezaji wote tegemeo wanaondoka wengine wakiuzwa na wengine mikataba ikiisha bila kuongezwa....jamani jamani hebu harakisheni kuokoa hali.....maumivu yanaendelea....hakuna habari njema wiki hizi mbili na mwezi mzima wa 5. Rekebisheni hali kwa kusajili at least mikataba ya awali ili kutoa moyo na kutia hamasa kwa wapenzi kuendelea kuchangia.....ukimya huu unaogopesha na ni hatari....mmeshaijenga chuki kwa wanayanga kuna wadau wa Yanga hawajitokezi kusaidia kwa kuwa tu hakuna dalili za kuanza kuleta mashine za uhakika hakuna hata mikataba ya awali kwa washambuliaji wakali na viungo wakali au mabeki wakali....Kuna kundi kubwa limeandaa fujo hawa ni wanachama ambao hawapendi hizi habari za huzuni zinazoendelea (Ajibu anaondoka burr, Makambo anauzwa, wachezaji 7 wanaumwa kuikosa Mbeya City, ubingwa kuchukuliwa na Simba, Sportspesa kuileta Sevila kucheza na Simba na siyo Yanga...nk. Na habari mbaya ndio zinazoendelea) Sasa amani ya nchi itavurugika....kwa kuwa kuna watu wanaumizwa na hizi habari...

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic