June 3, 2019

IMEELEZWA kuwa mlinda mlango wa Mbao FC, Metacha Mnata amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Yanga.

Yanga kwa sasa ipo kwenye mpango wa kusuka kikosi kipya kwa ajili ya msimu ujao ambapo kwenye sekta ya mlinda mlango walikuwa na tatizo baada ya Beno Kakolanya kuvunja mkataba hivyo Klaus Kindoki alikuwa bado ana makosa mengi ya kiufundi.

Metacha ambaye alikuwa Mbao kwa Mkopo akitokea Azam FC, mkataba wake tayari umeisha na kikosi chake cha Azam.


Mwenyekiti wa Mbao Solly Njash amesema kuwamkataba wao na Mnata ulikuwa ni wa mkopo hivyo bado alikuwa ni mali ya Azam FC na kama anakwenda Yanga itakuwa ni mipango yake mwenyewe.

"Mnata alikuwa nasi ametimiza majukumu yake vizuri hivyo mkataba wake nasi umekwisha kama amekwenda kujiunga na Yanga ni maamuzi yake pamoja na timu yake ya zamani, sisi tunamtakia kila la kheri," amesema.

2 COMMENTS:

  1. Yanga mnasajili tu pesa za kamati zikiisha mmeandaa vyanzo vingine?

    ReplyDelete
  2. Mabakuli yapo na yataendelea wanayanga wapo tayari Kwa Hali na mali mpaka ubingwa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic