July 30, 2019

ANWAR Binde, Ofisa Habari wa klabu ya KMC amesema kuwa kwa sasa vijana wanazidi kutengamaa kuelekea mchezo wao wa kimataifa dhidi ya AS Kigali.

KMC itamenyana na AS Kigali, Agosti 10 nchini Kigali ukiwa ni mchezo wa awali kwenye michuano ya kombe la Shirikisho.

Akizungumza na Saleh Jembe, Binde amesema kuwa mazoezi wanayoyafanya wachezaji wao yanawaimarsha kila siku.

"Kwa sasa tupo kwenye maandalizi kuelekea kwenye michuano ya kimataifa na vijana wanaonyesha utofauti kila iitwapo leo.

"Dozi ya asubuhi na jioni wanayoipata pale Uwanja wa Bora inawajenga hivyo matumaini makubwa ni kufanya vema kwenye mchezo wetu huo," amesema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic