NAHODHA
Msaidizi wa Yanga, Juma Abdul kwa sasa inaelezwa yupo kwenye mgogoro na mabosi wake
hao kutokana na madai yake ya stahiki
zake tayari Polisi Tanzania iliyo chini ya Kocha Mkuu, Seleman Matola inampigia
hesabu.
Habari
zinaeleza kuwa kwa sasa tayari mazungumzo ya awali yamefanyika na Polisi
Tanzania wanajitahidi kukimbizana na muda kabla ya dirisha kufungwa.
“Dirisha la
usajili linafungwa Julai 31 hivyo uongozi wa Polisi Tanzania unapambana
kukamilisha dili la Abdul atue ndani ya kikosi,” kilieleza chanzo hicho.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakalebela amesema kuwa bado hajapata taarifa kamili kuhusu mchezaji huyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment