August 19, 2019



JUZI Azam FC, ilishuhudia wapinzani wao Simba wakitwaa taji la Ngao ya Jamii kwenye mchezo wa ufunguzi wa Ligi Kuu uliochezwa Uwanja wa Taifa ikiwa ni mchezo wa 12 kuchezwa tangu kuazishwa michuano hiyo mwaka 2001.

Azam FC imeweka rekodi ya kibabe baada ya kushirki mashindano hayo mara sita na kutwaa taji moja tu ambapo mwaka 2012 ilifungwa 3-2 mbele ya Simba, 2013 ilifungwa bao 1-0 dhidi ya Yanga, 2014 ilifungwa mabao 3-0 dhidi ya Yanga, 2015 ilifungwa kwa penalti 8-7 dhidi ya Yanga baada ya dakika 90 kutoka sare ya bila kufungana.

Mwaka 2016 ilifanya maajabu kwa kushinda kwa penalti 4-1 mbele ya Yanga baada ya dakika 90 kutoka sare ya kufungana mabao 2-2 na mwaka 2019 kupoteza kwa kufungwa mabao 4-2 dhidi ya Simba uwanja wa Taifa.

Ettiene Ndayiragije, Kocha Mkuu wa Azam FC amesema kuwa wameshindwa kupata ushindi mbele ya Simba kwa kushindwa kutumia nafasi ambazo wamezipata kwenye mchezo huo.



2 COMMENTS:

  1. Yanga ndiyo walikuwa na Bahati! Simba wak vizuri sio barato hata kidogo!Azam imecheza na timu ambayo iko vizuri

    ReplyDelete
  2. Adam hawana bahati? Nafikiri!karibu Mara zote Tisa walikuwa wakicheza na favorites au more organized teams!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic