Wakati Manchester United wako katika juhudi kuu
kuhakikisha wanambasa Pedro Rodriguez wa Barcelona, wapinzani wao wakubwa Manchester
City nao wameingia vitani.
Man City wameingia vitani wakitaka kumpata nyota huyo
huku kukiwa na taarifa nyingine pia wanamhitaji Karim Benzema ambaye anatakiwa
na Arsenal.
Tayari Pedro amesema anaweza kuondoka Barcelona kwa
kuwa inaonekana haelewani na Kocha Louis Enrique lakini uamuzi wa City kuanza
kumfuatilia unaamsha vita mpya kabisa.
Tayari Man United iko tayari kutoa pauni milioni 22
kumpata, kuingia kwa City kunaweza kusababisha kupanda kwa bei ya kiungo huyo
mwenye miaka 28.
Man United inataka kumchukua kwa lengo kuziba nafasi
ya Angel Di Maria ambaye amekwenda PSG.
Pedro ndiye alikuwa shujaa wa Barcelona baada ya
kufunga bao lililoipa Barcelona ubingwa wa Uefa Super Cup kwa kuichapa Sevilla
kwa mabao 5-4.
0 COMMENTS:
Post a Comment