August 17, 2019


JOKATE Mwegelo anayeiwakilisha serikali kama Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Tawi la Yanga, Mlipo Tupo lililopo Kisarawe mkoani Pwani.

Jakate atazindua tawi hilo lenye wanachama zaidi ya 100 ambalo litakuwa la kwanza kuzinduliwa Kisarawe.

Katibu wa tawi hilo, Abdallah Muga amesema kuwa pamoja na uzinduzi wa tawi hilo kutakuwa na zoezi la ugawaji wa kadi kwa wanachama wapya na kusajili wapya na kumtunuku Kocha Mkuu, Mwinyi Zahera nishani ya uvumilivu kwa kuiongoza timu hiyo msimu uiopita.

"Tumewaalika viongozi mbalimbali wa ngazi ya juu lengo likiwa ni kumpa kocha Zahera tuzo ya nishani kwani msimu uliopita wakati kikosi kikiwa kwenye hali mbaya yeye alipambana na matarajio yetu mgeni rasmi awe Mkuu wa Wilaya, Jokate Mwegelo," amesema.

1 COMMENTS:

  1. Sishangai yanayotokea Yanga kwenye mechi za kirafiki na za mashindano ya CAF nilishashauri huko nyuma kuwa Yanga inahitaji kuliimarisha benchi la Ufundi kuongeza ujuzi na mbinu kwani viwango vya wachezaji vinaporomoka kwa kiwango cha juu mno....uwezo wa benchi la ufundi la Yanga ni mdogo mno...na kama hatua za haraka hazitachukuliwa kuliimarisha benchi la ufundi kuna hatari sana huko mbele aibu itatokea...Mimi si tu kwamba ninatathmini mchezo wa soka kwa umahiri ninazichambua timu kutokana na mechi zinazocheza.....nilisema kuwa Yanga inahitaji kuiiga Simba kutafuta Kocha Msaidizi kutoka Ulaya au Hata Amerika Kusini au Asia au Hata Africa mwenye viwango vya FIFA....ili wachezaji waongezewe mbinu katika mashindano.....Bado Yanga wana wachezaji wazuri lakini soka wanalocheza watapata tabu wakicheza na timu zenye mbinu za kubadilisha mchezo haraka.....kwahiyo hili la kubadilisha au kuliimarisha benchi la ufundi haliepukiki

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic