September 13, 2019



LEO Simba inatupa kete yake ya pili kucheza na Mtibwa Sugar na ilikuwa ikifanya mazoezi yake Viwanja vya Gymkhana pamoja na jana uwanja wa Uhuru ilikuwa ni mazoezi ya mwisho.

Leo kutakuwa na sapraizi kubwa kwa Mtibwa Sugar kutokana na sura nyingi za kazi kupewa nafasi ya kuanza kutokana na mazoezi ambayo Kocha Mkuu, Patrick Aussems aliwapigisha vijana wake.

Kwenye mchezo huo mpaka sasa inaonekana kwamba Aussems atapangua kikosi kitakachoivaa Mtibwa ambapo kwenye vikosi viwili vya alivyotumia kikosi cha kwanza kilikuwa kinaundwa na Aishi Manula ambaye ni mlinda mlango na upande wa mabeki ilikuwa ni Erasto Nyoni, Mohamed Hussein, Yusuph Mlipili, Shomari Kapombe, Fraga Vieira, kwa upande wa viungo ni Mzamiru Yassin, Hassan Dilunga, Clatous Chama, Shiboub na mshambuliaji alikuwa ni Miraji Athuman.

Kwa upande wa kikosi cha pili kiliundwa na Beno Kakolanya ambaye alikuwa ni mlinda mlango kwa upande wa mabeki Pascal Wawa, Haruna Shamte, Kennedy Juma na Gadiel Michael upande wa viungo wakiwa ni Jonas Mkude, Said Ndemla, Ibrahim Ajibu, Francis Kahata na kwa upande wa washambuliaji ikiwa ni Deo Kanda na Rashid Juma.

Mwishoni baada ya dakika tisini alimfanyia mabadiliko Jonas Mkude na Fraga Vieira, Tshablala alichukua nafasi ya Gadiel.

Sura mpya ambazo huenda zikaonekana leo ni pamoja na Rashid Juma, Said Ndemla, Haruna Shamte, Kenedy Juma na Yusuph Mlipili ambao wamekuwa hawapati nafasi mara kwa mara ndani ya Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic