October 2, 2019


MABONDIA wa ngumi za kulipwa nchini, Issa Nampepeche na Ally Hamisi wanatarajia kupima uzito kesho tayari kwa pambano la usiku wa mabingwa litakalofanyika Oktoba 4, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Club 361 uliopo Mwenge, Dar.

Mbali ya mabondia hao wengine watakaopima uzito kwa ajili ya pambano  hilo ni  Said Sudi atakayezichapa na Maganga Kulwa, Ibrahim Makubi  dhidi ya Abdallah Kingolwira, Hashimu Msungo vs Epson Lewis  wakati Salumu Omari atamalizana na  Ramadhani Chicho huku yakiwa chini ya udhamini wa  Gazeti  la Championi, +255 Global radio, Smart Gin, Glady Matata na Kiwango Security.

 Akizungumza na Championi Jumatano, mratibu wa pambano hilo, Seleman Semunyu alisema kuwa maandalizi ya kuelekea katika pambano hilo yamekamilika ambapo kesho mabondia wanatarajia kupima uzito kwenye Ukumbi wa Club 361.

 “Maandalizi yanakwenda vizuri kwa mabondia wote ambao watapanda ulingoni siku hiyo ambayo itakuwa ni kazi moja tu ya kuwapongeza mabondia wetu ambao wamechukua mikanda ya ubingwa nje ya mipaka ya Tanzania.
 
“Uzito tumepanga wapime kesho Alhamis kabla ya siku ya Ijumaa ambayo mabondia wenyewe ndiyo watapanda ulingoni, kikubwa mashabiki wa mchezo wa ngumi za kulipwa wajitokeze kwa wingi siku hiyo kushuhudia ngumi zikifanyika katika ustarabu wa hali ya juu kwa kiingilio kidogo,” alisema Semunyu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic