October 2, 2019



ZUBER Katwila, Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 20 amesema kuwa wachezaji wapo sawa kwenye mchezo wao wa leo dhidi ya Sudan.

Michuano hii ya CECAFA inafanyika nchini Uganda inaendelea leo na Tanzania ilitinga hatua ya nusu fainali kwa kuinyoosha Uganda jumla ya mabao 4-2.

Katwila amesema kuwa ana imani na vijana watapata matokeo chanya hivyo mashabiki wazidi kuwaombea.

"Maandalizi yetu yapo sawa na imani ni kubwa kwa vijana kufanya vizuri tunaomba mashabiki waendelee kutuombea kwani malengo yetu ni kupata ushindi kwenye kila mchezo," amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic