October 13, 2019



HASSAN Mwakinyo, bondia namba moja kwa Afrika kwenye uzito wa Super Welterweight kg 69 na namba 19 duniani amesema kuwa hana mashaka na mabondia kutoka Uingereza wala Marekani ambao wamekubali kupanda ulingoni kwenye pambano la World Class Fight Tanzania.

Pambano hilo linatarajiwa kufanyika Octoba 26 uwanja wa Taifa na litarushwa mubashara kwenye baadhi ya vituo vya Televisheni vya Bongo na vile vya nje kutokana na heshima ya Mwakinyo.

Akizungumza na Kijiwe cha Ndondi, Mwakinyo alisema kuwa anatambua kwamba Waingereza na mabondia kutoka Marekani wamepania kupambana naye jambo linalomfanya ajifue zaidi.

“Wanajua aina ya bondia wanayekwenda kupambana naye ana uwezo wa aina gani hivyo nao wanajipanga kuonyesha uwezo wao nitawaumbua mapema kabisa kwani nitakuwa nyumbani na mashabiki wangu, hili litakuwa pambano langu la kwanza nyumbani ni lazima nifanye mambo makubwa.

“Kuhusu kutaja majina yao kwa sasa naliacha suala hilo kwa mashabiki, kikubwa sapoti ni muhimu kwa mashabiki,” amesema Mwakinyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic