October 3, 2019



UONGOZI wa timu ya Polisi Tanzania umesema kuwa wachezaji wake wote leo wataogelea minoti na zawadi za kutosha endapo wataifunga timu ya Yanga ambayo mlinda mlango wao namba moja na Metacha Mnata.

Polisi Tanzania inacheza leo na Yanga uwanja wa Uhuru ikiwa ni mchezo wao wa tatu msimu huu, imeshinda mmoja mbele ya Coastal Union na kupoteza mchezo mmoja mbele ya Ruvu Shooting.

Habari zinaeleza kuwa wachezaji wote wamewekewa mezani dau lisilopungua la kutosha mezani kwa ajili ya kuwapa motisha kuwamaliza wapinzani wao leo.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Polisi Tanzania, Frank Lukwaro amesema kuwa wamejipanga kuona wachezaji wanachekelea ushindi wao mbele ya Yanga.

“Tunajua tunacheza na timu ngumu na kubwa jambo lililotufanya tuwaandae wachezai wetu kisaikolojia na wanatambua kwamba kuna zawadi zao ambazo tutawapa wakishinda, “ amesema Lukwaro.


4 COMMENTS:

  1. Yaani Polisi wanaahidi zawadi kwasababu wanacheza na Yanga, kwanini hawakuahidi kutoa zawadi wakicheza na Ruvu Shooting au Mbeya City???? Yaani hizi ni sababu kwanini mpira wetu haukui kwani Viongozi wanaopewa dhamana hiyo wana mawazo potofu na wanawalemaza wachezaji kwa ahadi za pesa kwaajili ya mechi 1 katika 38 za ligi mwishowe timu inashuka daraja kwani walikamia mechi 2 za Yanga na Simba tu msimu mzima

    ReplyDelete
  2. kama yanga akizubaa apigwe tu, maana kila timu inatafuta matokeo

    ReplyDelete
  3. Nasikia kila mmoja kaahidiwa boda boda,duh

    ReplyDelete
  4. pesa zinatoka simba hivyo hutoona wakiahidiwa pesa pale wanapocheza na simba
    sababu yanga hawana pesa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic