November 12, 2019



JUMA Mwambusi, Kocha Mkuu wa Mbeya City amesema kuwa licha ya kikosi chake kuwa na mwendo wa kusuasua kitarejea kwenye ubora wake.

Mbeya City imecheza jumla ya mechi 10 ina pointi 8 imeambulia ushindi mechi moja pekee na kupata sare tano vichapo mechi nne ikiwa nafasi ya 18.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mwambusi amesema kuwa ni suala la wakati kwa timu yake kurejea kwenye ubora kwani kwa sasa anapitia kipindi cha mpito.

“Tunapitia kipindi kigumu cha mpito kutokana na kutengeneza timu upya, wachezaji wana uwezo na ninawaamini katika kupambana kupata matokeo.

“Kumekuwa na shida kwenye safu ya ulinzi pamoja na ushambuliaji kwa kuwa matatizo tumeyatambua tutatumia muda mwingi kujiaandaa kwa ajili ya mechi zetu zinazofuata,” amesema Mwambusi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic