Ole Gunnar Solskjaer kocha mkuu wa Manchester
United amesema kuwa hajashtuka kufutwa kazi kwa kocha wa Tottenham Mauricio Pochettino ambaye amefutwa kazi
ndani ya kikosi hicho kutokana na mwenendo mbovu wa kikosi hicho.
Manchester United inaelezwa kuwa wameanza
kuiwinda saini ya Pocchetino ili awe bosi wao mpya ndani ya kikosi cha
Manchester United kilicho chini ya Solskjaer kwa sasa.
“Kufukuzwa
kwake ndani ya Tottenham hakujanishtua kwa sasa kwani alikuwa anafanya kazi
zake nami pia nafanya kazi zangu kwa sasa nimefanya kazi kwa umakini na
nimekuwa bora katika kile ninachokifanya.
“Haijalishi
ni nini kimetokea kwake na nini ambacho mimi nakifanya bado nitaendelea kufanya
vizuri na kupambana kwa ajili ya timu yangu, nimeona amepewa kazi Mourinho ninamtabua na uwezo wake ni mkubwa,” amesema.
Manchester
United kwenye Ligi Kuu England ipo nafasi ya 7 ikiwa imecheza jumla ya mechi 12
imejikusanyia jumla ya pointi 16 ikiachwa kwa pointi 18 na kinara wa ligi
ambaye ni Liverpool.
0 COMMENTS:
Post a Comment