JOTO la
mechi ya watani linazidi kupanda kwa sasa ambapo kila mchezaji na benchi la
ufundi wa timu hizi mbili hawana kingine wanachofikiria kwa sasa zaidi ya kuona
ni namna gani watatoka baada ya dakika tisini kupita Januari 4,2020.
Leo, Januari 3 yammebaki masaa kadhaa kabla ya watani hawa kumenyana pale uwanja wa taifa na miongoni
mwa wachezaji ambao wanakipiga Simba yupo beki mpya, Gadiel Michael ambaye
alijiunga na Simba akitokea Yanga kwa kadandarasi ya miaka miwili anatambua
joto lake kwa sasa.
Championi
Jumatatu limefanya mahojiano naye kuhusu namna anavyokiona kikosi chao cha
Simba pamoja na maandalizi kuelekea kwenye mechi hiyo pamoja na nyingine ambazo
zinawahusu wakiwa ni mabingwa watetezi huyu hapa anaanza:-
“Nimekuwa
kwenye masiha ya soka la ushindani kwa muda mrefu na inanifanya nakuwa bora
siku zote kutokana na muda ambao nimecheza jambo ambalo linanifanya nizidi
kupambana siku zote nje na ndani ya uwanja.
Kipi
kinakufanya usichuje?
“Nidhamu
katika kila jambo ambalo ninalifanya na kutambua nini ambacho ninakitaka na kwa
wakati gani ambao ninafanya.
“Katika kila
ambacho ninakifanya ninamtanguliza Mungu ambaye yeye ni mpaji wa yote jambo
ambalo linanifanya niwe kwenye ubora wangu muda wote.
Unaitazamaje
Simba?
“Ni timu ya
kipekee ndani ya Bongo imejipanga katika kila idara kuanzia uongozi na
wachezaji wote wanatambua wanatakiwa kufanya nini na kwa wakati gani wafanye
hayo mambo jambo ambalo linaifanya iwe hapa ilipo kwa sasa.
Ulikuwa
Yanga na sasa Simba kwa nini?
“Maisha ya
mchezaji na kazi anayofanya havimfanyi awe wa muda wote sehemu moja kwa wakati
wote. Mchezaji anaweza kuhama timu moja kwenda timu nyingine kulingana na
makubaliano na hicho ndicho kilichonitoa ndani ya Yanga na sasa nipo Simba
naendelea kupambana.
Kuna kitu
cha upekee ndani ya Simba?
“Ipo kuna
upekee katika maisha hasa ukiangalia namna ambavyo ninaishi na wenzangu ndani
ya Simba. Hapa sisi ni familia moja na kila mmoja anafanya jambo lake akitambua
ni la familia.
Uzito wa
mechi zenu za ligi upoje?
“Kila mechi
ni ngumu na wachezaji wanatambua kazi ya kufanya tunashirikiana katika kila mechi na kupeana
majukumu ya kufanya hilo linatufanya tuwe tunapata matokeo kwenye mechi zetu tunazocheza.
Mechi yenu
dhidi ya Yanga unaitazamaje?
“Ni mechi
ngumu na kila mmoja anatambua kwamba kila tunapokutana na timu yoyote
tunahitaji pointi tatu ambazo zitatufanya tufikie malengo yetu
tuliyojiwekea.Tunawaheshimu wapinzani wetu na tunajua kwamba ni timu bora ila
tutapambana ticheze tukiwa ni timu kwani tunazitaka pointi tatu zao ni muhimu
kwetu kama ilivyo kwao.
Unadhani
kuondoka kwako Yanga kumekuingiza kwenye uadui?
“Hapana,
sina ugomvi na Yanga nina marafiki zangu pale nab ado tunawasiliana nao kwani
mpira sio vita. Vita yetu sisi ni ndani ya uwanja baada ya hapo maisha
yanaendelea ndivyo ilivyo duniani kote.
Unajutia
kuondoka Yanga?
“Ni maamuzi
yangu mwenyewe kuondoka sikulazimisha, hapa nilipo nina furaha nitazidi
kupambana muda wote.
Vita yako na
namba na Tshabalala ipoje?
“Naipenda na
ni nzuri kwani hata nilipokuwa kulikuwa na ushindani wa namba. Kuhusu kuanza
ama kutoanza hilo mimi silijui lipo mikononi mwa mwalimu.
Unafanyaje
kuwa bora?
“Mazoezi na
kujituma ndani ya uwanja pale ninapopata nafasi na kucheza kwa juhudi nikiwa
mazoezini hata kwenye mechi pia,” anamalizia Gadiel.
0 COMMENTS:
Post a Comment