January 29, 2020



MWAKA 2019 umeshameguka na sasa tupo mwaka 2020, leo ni Januari,29. Haya hapa ni matukio ya StarTimes 2019:-

Tangu kuingia katika soko la Afrika Mwaka 2018, StarTimes  inajitahidi kufikia Malengo yake, ili kuhakikisha kwamba  kila Familia ya Kiafrika inapata,nafasi na uwezo wa kuangalia/Kutazama Televisheni ya Kidigitali.

Na hivi sasa StarTimes inatoa huduma kwa  watu takribani Milioni 30 katika nchi 37. Ukuaji huu mkubwa umeifanya  StarTimes kuwa muendeshaji mkubwa wa runinga  Barani Afrika na pia katika kuhakikisha inaleta maudhui mazuri kwa wateja wake.

StarTimes imetoa kipaumbele kwa jamii katika kuhakikisha inarudisha kile inachopata hasa katika kuunga mkono Taasisi zisizo  za kiserikali, Sekta ya Filamu Afrika.

Mwaka 2019 StarTimes ilitoa mchango wake  kwa Jamii katika haya:-
 
UCHANGIAJI

Polisi

Kampuni ya StarTimes Ilichangia Polisi vifaa vya Michezo ikiwemo Tshirt. Hii ilikua  katika kuchangia jamii na kusaidia mahitaji mbalimbali.

Tokomeza Ziro

Vile vile StarTimes ilichangia Elimu katika kampeni ya TOKOMEZA ZERO, Kisarawe kiasi cha Shilingi Milioni 10 katika kusaidia Serikali kwenye jitihada za kuhakikisha inatokomeza Zero.

Afya

Pia iliweza  kuchangia kiasi cha Shilingi Milioni 4 kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Cardiac Institute at Muhimbili National Hospital. Pesa hizo zilitolewa kusaidia Matibabu pamoja na huduma nyingine kwa watoto wenye matatizo ya Moyo.
 
HUDUMA KWA JAMII

StarTimes iliweza kutembelea kituo cha watoto yatima kitwacho (CHAWAMA ) kilichopo Sinza ,na kuwapatia msaada  kiasi cha Shilingi Milioni 3.

Kwa Upande wa Tamthilia mwaka 2019 StarTimes iliweza kuleta Tamthilia ya Waaris yenye maudhui yaliyopendwa  na watazamaji wengi na imejichukulia umaarufu sana ikifuatiwa na Wild Flower, Blood Sister na The queen of Flow.

UDHAMINI

Mwaka 2019,StarTimes waliweza kudhamini tamasha la wasafi lililofanyika katika mikoa mitano na kumalizikia jijini Dar es Salaam, ilifanikiwa kudhamini mashindano ya kusaka vipaji ya Bongo Star Search ambayo yalikwenda vizuri na kuhitimishwa vizuri.
 
MATUKIO

StarTimes iliweza kufanya matamasha ya kuleta wasanii wa tamthilia ya Ode to Joy  iliyofayika  katika Hotel ya Hyatty iliyopo Posta jijini Dar es Salaam.
ni wasanii maarufu sana nchini China,Tamthilia hii iliweza kufanyiwa tafsiri kwa lugha ya Kiswahili. 

TUZO

StarTimes imekabidhiwa TUZO  kutoka Shirika la TACAIDS  Tanzania kwa kutambua mchango wao StarTimes nao wakatoa mchango wa shilingi Million 5 ilikusaidia  Serikali katika mapambano dhidi ya  kutokomeza virusi vya Ukimwi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic