Timu ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 20 leo imeibuka na ushindi wa
mabao 2-1 dhidi timu ya Taifa ya Uganda kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa
Taifa.
Mechi ya leo ilikuwa ni ya kufuzu Kombe la Dunia litakalofanyika
Costa Rica na Panama, Julai 2-22 ambapo zilikwenda sare
Kipindi cha
pili kilianza kwa kasi kwa timu zote kutafuta ushindi ambapo Uganda ilianza
kupata bao la kuongoza kupitia kwa Nalukenge Juliet dakika ya 47 lililoongeza
kasi kwa timu ya Tanzania na kuwafanya wasawazishe dakika ya 58 kupitia kwa
Diana Lucas akimalizia pasi ya Asha Masaka.
Uzembe wa
mabeki wa Uganda dakika ya 68 uliwapa zawadi ya kona Tanzania iliyopigwa na
Diana Lucas na ikazamisha kimiani na Opah Clement.
Mechi ya marudio inatarajiwa kuchezwa Februari, Mosi nchini Uganda.







0 COMMENTS:
Post a Comment