TANGU Machi
17, mwaka huu lilipotoka tamko la Serikali kuzuia mikusanyiko isiyo ya lazima
na kusitisha shughuli mbalimbali ikiwemo michezo kutokana na janga la Virusi
vya Corona, kuna maoni mbalimbali yamekuwa yakitolewa.
Tamko la
Serikali ni ndani ya siku 30 ndiyo marufuku hiyo itatakiwa kufuatwa, lakini pia
itaangalia na namna hali ya hewa itakavyokuwa kwa maana ya hivyo virusi
vitakuwaje maambukizi yake.
Kusimamishwa
kwa michezo kumezifanya ligi zetu kusimama, hii si Tanzana tu, bali ulimwenguni
kote kwa sasa. Hapo awali ilikuwa kwa baadhi ya nchi, lakini sasa ni kote.
Bado
hatujafahamu siku sahihi ambayo ligi yetu itaendelea, lakini kwa taarifa za
awali hizo siku 30 zilizotolewa awali ni sehemu ya kuangalia namna tatizo
litakuwaje.
Lakini
upande mwingine kuna watu wamekuwa wakitoa maoni kwamba ni bora msimu huu
ufutwe, tuanze upya msimu ujao.
Ni mawazo ya
mtu au watu fulani ambayo kufuatwa ni uamuzi wa wenye mamlaka, lakini si vibaya
kuyachukua mawazo hayo.
Katika namna
ya kutoa uamuzi, suala hilo lipo chini ya mamlaka husika kwa maana ya
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambalo lina kamati zake zinazosimamia ligi
zetu.
Pia kama
tatizo hili litaendelea kuwepo siku zaidi ya zile ambazo zimetolewa awali kama
angalizo, basi uamuzi wa busara uchukuliwe. Iwe kuufuta msimu au kuamua ligi
zimalizike kwa staili gani.
Tusifuate
mkumbo wa wenzetu wamefanya nini, kisha sisi tukapita mulemule. Tunapaswa kuwa
na kauli yetu kama sisi Watanzania, wala tusiangalie wengine walichofanya.
Nimesikia
Ubelgiji hatua ambayo wamefikia ni kuufuta msimu hapo ulipofikia na kumpata bingwa.
Kwetu hatujafikia hatua hiyo.
Kama
ikifikia hatua hiyo, tuangalie namna itakavyokuwa. Wale waliokuwa wanakaribia
kupanda daraja, kuwa mabingwa na kushuka daraja itakuwaje.
Mfano msimu
ukifutwa hapa ulipofikia, kisha ikachukuliwa msimamo ulivyo kutafuta mshindi na
wa kushuka daraja, zipo timu ambazo zitaumia.
Kwa ligi kuu
pekee, Simba inaonekana kuwa karibu kuwa bingwa, Singida United ipo karibu
kabisa kushuka daraja.
Ligi Daraja
la Kwanza Kundi B, Gwambina imebakiwa na pointi tatu tu ipande daraja, lakini
pia kuna timu zipo kwenye hatari ya kushuka daraja.
Kwa mfano wa
ligi hizo mbili, ikichukuliwa uamuzi wa ligi kufutwa kisha wahusika wakasema
misimamo kama ilivyo ndiyo iamue nani awe bingwa na nani ashuke daraja na
kupanda, wapo watakaoumia hasa wale ambao katika mechi zilizobaki walikuwa na
uhakika wa kushinda na kujinasua na janga la kushuka daraja.
Lakini
wakisema ligi zifutwe, kisha kila ligi msimu wake uanze upya, kuna timu ambazo
zimefanya vizuri msimu huu na kubakiwa na asilimia chache kufikia malengo,
zikashindwa kutamba tena msimu ujao, hapo zitadhulumiwa.
Mwisho
kabisa, wahusika ambao ni TFF ndiyo wenye kauli ya mwisho endapo hali hii ya
hatari itaendelea kuwepo hata baada ya muda uliopangwa kupita.
Kikubwa mimi
na wewe tuombe hili janga liondoke na mambo yaende kama zamani, sidhani kama
hakuna mtu aliyekuwa hajamisi kuona soka likichezwa. Wote tumemisi, basi tuombe
Corona iondoke, lakini pia tujikinge kwa kufuata maelekezo ya wataalamu tusiwe
waathirika.
kwa vyovyote itavyokua, ili haki itendeke kwa timu zote ni lazima mechi zilizobakia zichezwe pindi gonjwa la corona litaposepa zake hata kama ni mwisho wa mwaka
ReplyDeleteInahitaji busara kubwa Sana kwani zimebaki mechi tano tu za kujulikana bingwa baada ya wanaoongoza ligi na kut7umia mabilioni ya shilingi na jasho kubwa sana walilomwaga na kuwepo majeraha na maumivu yaliyochukuwa miezi kupona na kungojea baadhi mpaka leo hii kupona. Tunangojea busara isiyoleta maumivu kwa baadhi na kuwafurahisha baadhi kisicho tarajiwa kama ilivokuwa haikutarajiwa corona. Nchi nyingi zimeshatangaza kummaliza ligi Bila ya mashabiki ka vile Misri tangu karibu miaka mitano iliyopita
ReplyDeletetumalizie tu ligi bila mashabiki basi kama burundi
ReplyDelete