KAULI ya Kocha
wa Arsenal, Mikel Arteta, kuhusu kwamba hawezi kumbembeleza mchezaji kusalia
ndani ya klabu hiyo kama hana nia ya kuendelea kuwa hapo, moja kwa moja
inaelezwa imemlenga staa wa timu hiyo, Pierre–Emerick Aubameyang.
Kwa siku za
karibuni, Aubameyang ameonekana kugoma kusaini mkataba mpya ndani ya Arsenal
wakati ule wa awali ukitarajiwa kumalizika Juni, mwakani.
Wakati Aubameyang
akigoma kusaini mkataba huo, amekuwa akihusishwa kutakiwa na klabu kadhaa
ikiwemo Barcelona, Real Madrid na Manchester United.
“Siwezi kumshawishi
mchezaji kucheza Arsenal au kujiunga na sisi, mchezaji anatakiwa kujitoa na
kupambana kwa ajili ya klabu,” alisema Arteta alipoulizwa mipango yake ya
usajili na namna ya juhudi zake za kuwashawishi mastaa wasiondoke klabuni hapo.
Aende tu akatafute maisha mapya😊😊😊😊
ReplyDelete