KUTOKANA na hali ya ukata inayoikabili Ndanda FC, klabu hiyo imeliomba
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), liwakopeshe fedha zitakazowasaidia katika
uendeshaji ili kumalizia michezo iliyobaki ya Ligi Kuu Bara.
Ndanda ambayo imekuwa ikiendeshwa kwa michango ya wanachama na wadau,
mara kwa mara imekuwa na hali mbaya kiuchumi huku mara kadhaa wakikiri
kushindwa kulipa mishahara ya wachezaji wao.
Katibu Mkuu wa Ndanda, Selemani Kachele, amesema: “Tumesikia kuwa Ligi
Kuu Bara inaweza kurejea hivi karibuni kama hali ya mambo itakuwa vizuri, ni
jambo la kushukuru lakini sisi kama Ndanda hali yetu ya kiuchumi kwa sasa sio
nzuri.
“Kama mnavyojua kuwa klabu hii inaendeshwa kwa michango ya wanachama,
hivyo tunaiomba TFF na Bodi ya Ligi kama itafikia uamuzi wa kuirejesha ligi basi
watusaidie kutukopesha fedha zitakazotusaidia kuiendesha klabu yetu kumalizia
michezo iliyobaki.”
Katika
msimamo wa Ligi Kuu Bara, Ndanda inashika nafasi ya 16 baada ya kujikusanyia
pointi 31 katika michezo yake 29.
SOURCE: SPOTI XTRA
SOURCE: SPOTI XTRA
TFF inatakiwa kuwapa fedha timu zote kutoka mfuko maalum kwasababu FIFA inawapa fedha kila mwaka,labda tuu zinaenda kwa mchina.
ReplyDelete