May 7, 2020


MABOSI wa Simba wamesema kuwa wamemruhusu kiungo wao, Ibrahim Ajibu kuondoka muda wowote atakaohitaji na kwenda kujiunga na klabu nyingine itakayomuhitaji kwa masharti, ikiwemo Yanga.

Hii imekuja siku chache tangu taarifa kuzagaa kuwa mchezaji huyo anataka kuondoka kwenye kikosi hicho cha kujiunga na timu moja ya nje ya nchi.

Ajibu alijiunga na Simba msimu huu kwa dau la Sh Mil 80 akitokea Yanga mara baada ya mkataba wake wa miaka miwili kumalizika. Inaelezwa kuwa timu hiyo imemruhusu kiungo huyo kuondoka lakini lazima masharti maalum yafuatwe.

Mtoa taarifa huyo alisema kiungo huyo wakati anasajiliwa na Simba, viongozi walitegemea kuona makubwa kutoka kwake, lakini imekuwa tofauti baada ya staa huyo kupoteza nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza.

“Wakati anasajiliwa na Simba akitokea Yanga, mabosi walikuwa wana matarajio makubwa ya kumuona Ajibu akicheza kwa mafanikio katika msimu huu, lakini imekuwa tofauti na matarajio yao.

“Hivyo, viongozi wamepata taarifa za Ajibu kutakiwa na moja ya klabu kutoka nje ya nchi, hivyo uongozi umekubali kuachana naye kwani hayupo kwenye mipango ya kocha kuelekea msimu ujao, siyo nje tu ikija timu yoyote hata Yanga tunamruhusu.

“Kikubwa anatakiwa kufuata masharti ya klabu kwa kuiambia timu inayomtaka,”alisema mtoa taarifa huyo.

4 COMMENTS:

  1. Ajib ,yanga? Hapana hata bure ,yanga hii no level nyingine

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kipi cha ajabu ilichokifanya Yanga hiyo mpaka iwe level myingine Wabongo bwana kila best looser alafu yanga hii level nyingine ushubwada mtupu

      Delete
  2. Ajibu nisimba damu taarifa za kweli kuhusu ajibu hazitolewi na makanjanja,bali club ndio hutoa mustakbali wa mchezaji acheni kuropoka

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic