MTAMBO wa mabao ndani ya Kabu ya Mbao FC iliyo chini ya Kocha
Mkuu, Felix Minziro, WAZIR Jr amesema kuwa iwapo masuala ya michezo yatamzingua
ataibuka kupiga dili za masuala ya teknolojis ili kupiga mkwanja.
Jr ametupia mabao saba na kutengeneza asi mbili za mabao kati ya
19 ambayo yamefungwa na Mbao FC iliyo nafasi ya 19 na pointi 23.
Akizungumza na Spoti Xtra, Jr alisema kuwa mbali na kucheza
mpira ana ujuzi wa masuala ya IT jambo ambalo anaamini kuwa akibuma kwenye soka
atapiga hela upande huo.
“Ukiachana na soka mimi nina ujuzi wa masuala ya IT hivyo
ninadhani iwapo nitashindwa kuendelea kuwa kwenye masuala ya mpira basi
nitapiga madili ya teknolijia kwani huko ndiko ulimwengu ulipo.
“Ninachojua mimi ninaweza kufanya vyote kwa ukamilifu ila kwa
sasa nguvu kubwa nimewekeza kwenye masuala ya mpira wakati ukifika nitafanya
kazi niliyosomea darasani,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment