July 26, 2020

ASTON Villa inayoshiriki Ligi Kuu England ni miongoni mwa timu tatu ambazo leo zinapambana kujinasua kushuka daraja.

Timu nyingine ambazo zinaungana na Villa anakokipiga
nyota wa Tanzania, Mbwana Samatta ni pamoja na Watford na Bournemouth ambazo hazina uhakika wa kubaki ndani ya Ligi hiyo pendwa mpaka watakapokamilisha dakika 90.

Leo Jumapili, Julai 26 msimu wa Premier unafika tamati huku ule mpya wa 2020/21 ukitarajiwa kuanza Septemba 12.

Aston Villa ina pointi 34 ikiwa nafasi ya 17 itakuwa ugenini kucheza na West Ham United ambao hawana cha kupoteza na inatakiwa kushinda ama kuwaombea njaa wengine ambao ni Watford na Bournemouth wapoteze mechi zao.

Watford ipo nafasi ya 18 ikiwa na pointi 34 wametofautiana bao moja tu na Villa itamenyana na Arsenal huku Bournemouth ikiwa nafasi ya 19 na pointi 31 ina kazi mbele ya Everton na ina kazi ya kushinda kwa mabao mengi ili kuzipoteza zile zilizo juu yake.

Mechi zote leo zinatarajiwa kupigwa kuanzia majira ya saa 12:00 jioni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic