MSHAMBULIAJI wa Lipuli Daruesh Saliboko, amesema kuwa ataendelea kumuenzi hayati, Benjamin Mkapa, rais wa awamu ya tatu ambaye alifariki jana, Julai 24.
Kesho Julai 26 kwa mujibu wa Serikali kutakuwa na taratibu za kuuaga mwili wa Mkapa Uwanja wa Uhuru.
Akizungumza na Saleh Jembe, Saliboko mwenye mabao 11 kibindoni amesema kuwa enzi za uongozi wa Mkapa yeye alikuwa bado mdogo lakini ameshuhudia mengi yakitendeka.
"Zama za uongozi
wake nilikuwa mdogo sana lakini nilikuwa ninaona juhudi zake hasa kwa kuwa
karibu na jamii, pia nimekuwa mkubwa nimeuona Uwanja wa Taifa na nimeutumia pia
ni juhudi zake,ni pengo kubwa lakini sisi sote ni wa Mungu.”
0 COMMENTS:
Post a Comment