August 27, 2020


JUMA Abdul, beki wa zamani wa Klabu ya Yanga amesema kwa sasa anafikiria zaidi kucheza soka la kulipwa nje ya nchi na kuna dili analisubiri na kama likitiki tu anasepa.

 

Beki huyo mtaalamu kwa krosi amesema kwa sasa hajasaini timu yoyote hapa nchini labda dili lake la kwenda nje likwame ndipo anaweza kufikiria timu nyingine ya kwenda.


Akiwa Yanga msimu wa 2019/20 alitoa jumla ya pasi sita za mabao kwa mguu wake wa kulia aliachwa na Yanga baada ya kushindwana kwenye masuala ya mkataba.

 

Abdul pamoja na beki mwingine wa kati, Kelvin Yondani walitangazwa kuachwa na Yanga klabu ambayo waliitumikia kwa miaka nane. Ilidaiwa Yanga iliachana na wachezaji hao kwa madai ya kushindwana katika maslahi.

 

Hata hivyo kumeibuka maneno kuwa klabu hiyo imepanga kuwaita tena mezani wachezaji hao wazoefu ili kufanya nao mazungumzo ya kuwemo katika kikosi hicho msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

1 COMMENTS:

  1. Fanyenii nao mazungumzoo mapema ili waendelee kufanya mazoez kwa pamoja

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic