August 20, 2020

 

RATIBA ya Ligi Kuu England maarufu Premier League kwa msimu wa 2020/21, imetolewa leo Alhamisi ambapo mechi zitaanza kuchezwa Septemba 12, mwaka huu.

 

Ratiba hiyo inaonesha kwamba, siku ya ufunguzi zitachezwa mechi sita, kisha Septemba 14, zitachezwa mechi mbili.

 

Mabingwa watetezi wa Premier, Liverpool, wataanza kampeni ya kulitetea taji lao wakiwa nyumbani Anfield kupambana na timu iliyopanda daraja, Leeds United.

 

Wageni wengine wa ligi hiyo, Fulham watakuwa nyumbani kupambana na Arsenal. West Brom ni dhidi ya Leicester City.

 

Wakati wengine wakicheza wiki ya kwanza, mechi mbili ambazo ni Manchester City vs Aston Villa na Burnley v Manchester United zimesogezwa mbele kutokana na Man United na Man City kupewa muda zaidi wa kupumzika baada ya timu hizi hivi karibuni kutoka kwenye michuano ya Ulaya.

 

Manchester United na Manchester City, wenyewe wataanza kampeni zao Septemba 19, mwaka huu.

 

RATIBA KAMILI KWA WIKI YA KWANZA IPO HIVI;

SEPTEMBA 12

Crystal Palace  vs   Southampton

Fulham              vs   Arsenal

Liverpool           vs   Leeds United

Tottenham       vs   Everton     

West Brom       vs   Leicester City

West Ham        vs   Newcastle

 

SEPTEMBA 14

Brighton           vs   Chelsea

Sheffield           vs   Wolves

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic