September 29, 2020

 


BAO la faulo la kitasa wa Simba, Muivory Coast, Pascal Wawa, limemuibua kocha wa kikosi hicho, Sven Vandenbroeck kwa kusema kuwa alimisi kuona mabao ya aina hiyo kwenye timu hiyo.

 

Sven ameongeza kuwa aina ya mabao hayo ya mipira ya adhabu kwa kiasi kikubwa aliyamisi kuona yakifungwa ndani ya kikosi hicho kutokana na kupoteza nafasi hizo mara nyingi wanapopata.

 

Wawa alifunga bao lake la kwanza la msimu huu kwa faulo katika mechi dhidi ya Gwambina FC, kwenye mechi iliyopigwa Uwanja wa Mkapa, Dar, Septemba 26.

 

 Sven amesema kuwa licha ya uzuri wa bao hilo pia Wawa ni mfungaji mzuri wa mipira hiyo ambapo ameshawahi kufanya hivyo kwenye mechi zao za msimu uliopita.  

 

“Tulifunga kwa njia ya mipira ya adhabu, hiki ni kitu kizuri kwa sababu kwa muda mrefu hatukufunga, nafikiri hii ndiyo mara ya kwanza tumefunga kwa namna hiyo baada ya muda mrefu sana.

 

“Wawa (Pascal), anajua kupiga mipira hiyo ya adhabu, msimu uliopita kwenye mechi dhidi ya Azam FC na Yanga alichukua jukumu hilo la kupiga na kufanya vizuri. Lakini pia tuna wapigaji wazuri wa mipira hiyo akiwemo Miquissone (Luis) aliyepiga lakini kipa alitoa,” alimaliza Sven.

 

Katika mchezo huo, Simba walipata ushindi wa mabao 3-0 kwenye mchezo mkali uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa.


Simba kwenye msimamo wa ligi ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 10 sawa na Yanga iliyo nafasi ya tatu baada ya kucheza mechi nne huku vinara wakiwa ni Azam FC wenye pointi 12, Gwambina ipo nafasi ya 17 na pointi moja. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic