September 29, 2020

 


MKURUGENZI wa Ufundi wa Gwambina ambaye alikuwa Kocha Msaidizi wa timu ya Taifa ya DR Congo, Mwinyi Zahera, ametolea ufafanuzi suala la kuachwa kwa nyota wawili wa Yanga, Tuisila Kisinda na Mukoko Tonombe kwa kusema hawawezi kupata nafasi kwenye timu hiyo ya taifa.

 

Tuisila na Tonombe walijiunga na Yanga kwenye usajili wa dirisha kubwa mwaka huu wakitokea AS Vita ya DR Congo.

 

Zahera amesema kuwa nyota hao wa zamani wa AS Vita hawawezi kupata nafasi kwenye kikosi hicho kutokana na ushindani wa namba uliopo.

 

“Nimeona kikosi cha Timu ya Taifa ya Congo kilichoitwa hivi karibuni ili kujiandaa na michezo miwili dhidi ya Burkina Faso, Oktoba 9 na baadaye dhidi ya Morocco na najua watu wengi hasa mashabiki wa klabu ya Yanga wamekuwa wakijiuliza kwa nini nyota wao, Tuisila Kisinda na Mukoko Tonombe hawajaitwa.

 

“Hapa jibu ni rahisi tu, timu ya Taifa ya Congo ina wachezaji zaidi ya 400 ambao wanacheza barani Ulaya, yupo mchezaji anayecheza Ligi Kuu nchini Ufaransa ambaye anacheza nafasi moja na Kisinda naye hajaitwa kwenye timu kwa sababu wapo wachezaji wanaocheza kwenye nafasi zao walio kwenye ligi bora zaidi, hawa ndiyo wanapewa kipaumbele wakati wa kuita timu ya taifa.

 

“Ndiyo maana licha ya kwamba Tonombe na Kisinda wote wametoka As Vita ambayo ilikuwa inafundishwa na kocha wa timu ya Taifa ya Congo, lakini hawakuwahi kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa,” amesema Zahera.

 

19 COMMENTS:

  1. Utetezi wa kitoto sana. Sema tuu hawana uwezo huo.

    ReplyDelete
    Replies
    1. True! kweli wasipepese macho Wala wasitikise masikio, waeleze ukweli tu hawana uwezo hao wachezaji

      Delete
  2. Kwa maelezo ya kocha msaidiz wa timu ya taifa ya Congo MWINYI ZAHERA,Kumbe TONOMBE NA KISINDA hawajawahi kuitwa timu ya Taifa ha ha ha ha ha ha CHIRWA ameitwa.itabidi waitwe TAIFA STARS maana sifa tunazopewa kwamba wapo first eleven ya taifa sasa iweje??

    ReplyDelete
  3. Kwa hiyo Eng. Hersi alitudanganya kwamba ni wachezaji wa timu ya taifa ya DRC?

    ReplyDelete
  4. Naona wanangu wa msimbazi mnateseka Kwan mugalu ameitwa?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Majibu ya swali hilo kamuulize MWINYI ZAHERA au mjomba enu,ukweli utabaki palepale kwamba hawana uwezo wa kucheza timu ya Taifa,na hata aliposajiliwa CHIRWA pia tuliambiwa anachezea timu yake ya Taifa ila juzi kwa kinywa chake anasema ndio mara yake ya kwanza kuitwa kwenye timu ya Taifa na anaona fahari kuu,bado yaliyojificha yatajulikana muda sio mrefu japo tayari tunafahamu fika kwamba wapo hapo kwa mkopo

      Delete
    2. Dah! kula tano 👊 bonge la point, hili yawezekana likawa Kama la makambo.

      Delete
    3. Kwahyo kwaakili yko ulitaka iweje wawe kwamkopo wasicheze timu ya taifa we inakukera nini tunacho jua ni wachezaji wa yanga au ulitaka waitwe ili ufaidike nini ndo maana mnapigwa kumbe wambea hvo

      Delete
  5. Halafu Timu ya Taifa ya Congo DRC ni tofauti Sana na Zambia, Tanzania,Rwanda ,na sijui Kenya msilete Uswahili ndiyo maana Mugalu Chris Kaitwa ,Mikia hoyeeeee

    ReplyDelete
  6. Wapo kwa mkopo nao mnawavizia?Mwandae Hans Pope Tena Kamati ya maadili

    ReplyDelete
  7. Tatizo mikia mmesajili wachezaji ambao kwenye timu za taifa wanaocheza nje walio wengi ni Tanzania sasa kwann wasiitwe. Umeambiwa kuna mafundi wengi wapo ulaya kwenye ligi bora sasa hapo lipi hamjaelewa. Lakin wangekuwa wanatoka kwenye nchi ambazo ninyi mnasajili wangekuwa first eleven.

    ReplyDelete
  8. Zambia toka China anunue nchi mpira bye-bye eti Timu ya Taifa Zambia inategemea Chama wa Simba au Larry Bwalya ,hao na Zanzibar hapana tofauti.

    ReplyDelete
  9. Timu ya Congo ina mapro wengi wanakipiga ulaya, hii ligi yetu haiwezi kushindana na ligu za majuu, hao zambia wanawachezaji gani wanacheza ligi bora ulaya?
    Hakuna ndio maana unaona skina Chama wanaitwa.

    ReplyDelete
  10. Nyie mliambiwa mapema kabisa wale wanacheza timu ya taifa ya wachezaji wa ndani, yaani CHAN, Sasa mlitaka nini tena kama hamukuelewa mwanzo si mngeuliza?

    ReplyDelete
  11. Manyani mabishi kweli yanapoint za kijinga ili mradi yaonekane na yao yameongea

    ReplyDelete
  12. Basi Mugalu Kaitwa,ila mkubali Zambia kwishneeee.Huyo Bwalya Larry na Ndemla hapana tofauti
    Hapa kwetu Ndemla National Team hata hafikiriwi Sasa Zambia si ndo bye-bye?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic