UONGOZI wa Simba umesema kuwa suala la mchezaji wao wa zamani ndani ya timu hiyo Shiza Kichuya kufungiwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa, (FIFA) pamoja na wao kutakiwa kulipa faini ya dola za kimarekani 130,000( M.300) bado hazijafika mezani kwao.
Habari zinaeleza kwamba Kichuya aliyesajiliwa na Simba kwenye dirisha dogo msimu wa 2019/20 kwa dili la miezi sita bado alikuwa ni mali ya timu yake ya zamani ya Pharco ya Misri ambayo iliinasa saini ya nyota huyo kutoka Simba msimu wa 2018/19.
Nyota huyo alikuwa ameshitakiwa na Klabu ya Pharco ya Misri iliyoinasa saini yake msimu wa 2019 kutokana na madai ya kukatisha mkataba wake ndani ya timu hiyo kisha akajiunga na Simba Januari, mwaka huu.
Shauri hilo lilikuwa linafanyiwa uchunguzi na Kamati maalumu ya DR Congo iliyo chini ya FIFA kabla ya kutoka kwa maamuzi ya faini hiyo ya Kichuya kufungiwa.
Kaimu Mwenyekiti wa Simba, Mwina Kaduguda amesema:"Taarifa hizo bado ni mpya kwetu, Bodi ya Wakurugenzi hatujapokea taarifa rasmi kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wetu, Barbara Gonzalez, hivyo tunasubiri taarifa rasmi ifikishwe kisha tutakaa kuijadili.
"Ila tunawaomba mashabiki wa Simba wawe watulivu kwa sababu maamuzi kama haya yanafanyika lakini hayamaanishi kuwa yapo sahihi.
"Kuna wakati maamuzi yanaweza kufanyika na yasiwe sahihi na ndiyo maana ipo nafasi ya kuweza kukata rufaa na maamuzi yakabadilishwa baada ya kupitiwa upya, nisingependa kuongea mengi kwa sasa tusubiri Barbara atalitolea ufafanuzi," amesema.
Kwa sasa Kichuya anacheza ndani ya Namungo ambayo inashiriki Kombe la Shirikisho na Ligi Kuu Bara ikiwa chini Kocha Mkuu, Hemed Morroco.
Chanzo:Spoti Xtra







Unakata rufaa kwenda wapi kama fifa wameamua hill. Machen kuwapumbaza mashabiki.
ReplyDeleteUngenyamaza kama hujui kuna mahakama ya michezo cas unaweza kukata rufaa kama hukubaliani na maamuzi ya FIFA
DeleteNi kweli Rodrick, kama jambo hulijui...ni bora usilizungumzie. Vilabu vingi vya soka duniani na pia wanamichezo wengine kwa ujumla wanaitumia sana CAS.
DeleteHata maamuzi ya FIFA yaweza kukatiwa rufaa, ni katika Court of Arbitration for Sport (CAS). Hapo sasa ndio mwisho!
ReplyDeleteUkirejea Email iluyotumwa Namungo, uamuzi huu wa fine ya Dola 130,000, umetolewa na CAS. Ukiwahusu Simba, Kuchuya kutocheza kwa miezi 6 na Namungo kutomtumia hadi adhabu yake ilipwe.
ReplyDeleteKisichowazi ni hatma ya michezo aliyoshiriki Kichuya.
Hivi ninyi watu was Simba akili zenu na huyo anayenukuliwa kuongea zinatia huruma kwa taarifa yenu Kama huyo mchezaji angetoka Timu ya ndani TFF wangechezesha mtambo mala ungesikia usajili wa awali mkataba unatofautiana na ::::; ili mradi kusafisha usanii wa Simba ,refer Morrison Case,hogopa Timu inasajili asilimia 90 kwa kuchungulia wachezaji walomaliza mikataba .HILO MNALO hakuna Cha CAS Wala CUF Wala Nini punguzeni utoto wa mjini .
DeleteMkataba si upo na kucheza si alicheza... kukata rufaa ni kuijongezea gharama tu. FIFA sio fff.
ReplyDeleteHapa tungeshauri pointi zote Simba ilizopata wakiwa na huyo mchezaji wangenyanganywa kuwapa adabu ,hii haina tofauti na mechi fixing
ReplyDeletekichuya anapaswa kuwajibika kwa kusaini mkata na timuu nyingne huku akijua anamkataba na timu nyngne.
ReplyDeleteUnaweza kukata rufaa kama una uhakika na jambo unalolikatia rufaa,lakini kama huna uhakika ni kupoteza muda na kujitafutia matatizo makubwa zaidi.Kumbuka simba wamepewa siku 45 tu wawe wamelipa kiasi hicho cha pesa,vinginevyo watafungiwa kusajili wachezaji wapya kwa kipindi cha misimu miwili,sasa hapo ndo unapoweza kuona athari ya kukata rufaa pale utakaposhindwa kesi......nyie neng'enekeni tu na kujiongopea........hilo ni trela tu jiandaeni na picha kamili kwenye issue ya morrison.
ReplyDeleteSimba hawajakataa faini ila wamesema haijawafikia taarifa ya wao kulipa pesa mbona hamuelewi nyinyi utopolo?
ReplyDeletewewe mkia ndo huelewi na unapitwa na wakati,kabla ya hiyo taarifa ya simba unayoisema wewe walishasema kuwa watakaa kuona kama wanaweza kukata rufaa,.soma taarifa za jana.
DeleteWamesha Umia, hapo maamuzi yametolewa kwa uweledi mkubwa sio TFF wazee wa mbeleko, Kateni rufaa mzidi kukiwa,
ReplyDeletendio mjifunze sio deal kuzoazoa wachezaji ovyo...!
Pamoja na kutotumika, lkn Hiyo tafsiri yake thamani ya Kichuya ni zaidi ya 300M,
ReplyDeleteHasara ya kiwango cha lami
Ugumu wa hii, kuwa kipindi tunalopoka ugolo wetu huu, kumbuka Kichuya alikaa nyumbani zaidi ya miezi sita
ReplyDeleteYaani waandishi.wangetuletea mchanganuo,tupige hesabu wenyewe,ingekua poa sana.lkn tunajadili hukunu na hatujui mwenendo na hoja kesi.basi ni kutomboka tu
ReplyDelete