December 31, 2020

 


TANZANIA Prisons ikiwa Uwanja wa Nelson Mandela imelazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Yanga kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara wa mzunguko wa pili.


Kipindi cha kwanza timu zote mbili zilitoshana nguvu bila kufungana ndani ya dakika 45 za mwanzo za mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa.


Kipindi cha pili,Prisons walianza kupata bao dakika ya 52 kupitia kwa Jumanne Elifadhili.


Bao la kuweka usawa kwa Yanga lilifungwa na Saido Ntibanzokiza dakika ya 76 katika harakati za kuweka mzani sawa ndani ya uwanja.

Yanga imefunga mwaka 2020 ikiwa imecheza jumla ya mechi 18 vila kupoteza na kugawana pointi mojamoja na Prisons. 


Hili linakuwa ni bao la pili kwa Ntibanzokiza ambaye ni ingizo jipya, bao lake la kwanza alifunga mbele ya Dodoma Jiji.


Sare hiyo inaifanya Yanga kufikisha pointi 44 ndani ya Ligi Kuu Bara ikiwa nafasi ya kwanza baada ya kucheza mechi 18, Tanzania Prisons inafikisha pointi 22 ikiwa nafasi ya 9.

17 COMMENTS:

  1. Kila mtu ashinde mechi zake hatutasikia tena.Mambo yameanza kuwa magumu.Ligi ni marathon sio sprint.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nyie si mlikung'utwa?

      Delete
    2. Na kila mtu afungwe mechi zake

      Delete
    3. Fikiria endapo Yanga leo isingekuwa na wachezaji wake watano wa kikosi cha Kwanza, yaani Lamine,Saido, Sarpong, Tuisila na Mukoko..Ndiyo ilikuwa hivyo kwa Simba..Kikosi cha Yanga ni hicho hicho..iwe ihefu au polisi hata Azam

      Delete
    4. Ile kauli ya "Tuna kikosi kipana" imeyeyukia wapi?

      Delete
    5. BADO IPO SI UMEONA HAKUNA WAWA WALA MKUDE NANYONI IHEFU KALIWA 4.

      Delete
    6. Inategemeana lakin chama si alikuwepo baba yenu na uwanja haukuwa na tope Kama leo

      Delete
    7. Kwahiyo ninyi mnacheza kiangazi tu

      Delete
  2. Leo vipi mliogopa kutupa taarifa wakati mechi inaaendelea au tatizo nini?

    ReplyDelete
  3. Hata mimi nilishangaa hapakuwa na live updates, labda masharti ya mganga

    ReplyDelete
    Replies
    1. Inawezekana maana uto wanaamini Sana hizo Mambo, leo kila Mara walikuwa wanafukua kwenye goli la prison

      Delete
  4. Mtakeleka ha2japoteza mchezo litawachoma sana na ha2fungwi mlijua 2tafungwa ha2fungwi subirini mwakan 2wape dozi mikia nyie

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tatizo kipindi hiki ni masika na nyani hamuwezi kucheza kwenye uwanja uliyolowa maji, sijuwi mtafanyaje!!!

      Delete
  5. Wakipenda wakichukia, wakiandika wasiandike mnyama ana close in, anapiga hodi na milango imeshafunguliwa

    ReplyDelete
  6. Nguruwe fc mbona mnajifanya kuteseka hivi, au kisa mlibanjuliwa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic