January 21, 2021



KIKOSI cha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Klabu ya Simba kinatarajiwa kurejea rasmi kambini Januari 25, ambayo ni siku ya Jumatatu ya wiki ijayo.

Tangu kumalizika kwa michuano ya Kombe la Mapinduzi, kikosi cha Simba kilipoteza fainali ya michuano hiyo mbele ya Yanga kimekuwa kwenye mapumziko.

Inatajwa kuwa siku hiyo Simba inaweza kuanza rasmi mazoezi na kocha wake mpya ambaye yuko kwenye mchakato wa kutangazwa hivi karibuni, ili kujiandaa na michezo ya Ligi Kuu Bara pamoja na ile ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Simba inatarajiwa kuanza kibarua chake kwenye Ligi ya mabingwa Afrika Februari 12, mwaka huu dhidi ya AS Vita kutoka DR Congo. 

 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic