March 20, 2021


 

UONGOZI wa Simba umeweka wazi kuwa utapambana kutimiza agizo la Rais wa awamu ya tano, John Magufuli la kuwataka watwae ubingwa wa Afrika.

Agizo hilo alilitoa msimu wa 201//18 wakati akiwakabidhi ubingwa wa Ligi Kuu Bara na alishuhudia timu hiyo ikitunguliwa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar.

Magufuli ambaye alitangazwa kufikwa na umauti Machi 17 na Makamu wa Rais, Samia Suluhu ambaye kwa sasa ni Rais wa awamu ya sita aliweka wazi kwa kuwaambia Simba anahitaji kuona wakimuita akiwakabidhi Kombe la Afrika jambo ambalo halijatimia mpaka anafikwa na umauti.

Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema:”Rais wetu ameondoka ghafla na sisi Wanasimba tupo kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na tutashiriki kwa nguvu kubwa na ari ili kuenzi changamoto ambayo alituachia.

" Tukiwa ni Wanasimba, wanasoka agizo lake linapaswa lituongoze ili hatimaye tufanikiwe kubeba taji la ubingwa wa Afrika,” .

Kwa sasa Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes imetinga hatua ya makundi inaongoza kundi A ikiwa na pointi 10.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic