UONGOZI wa Klabu ya Njombe Mji inayoshiriki Ligi Daraja la
Kwanza umeweka wazi kuwa kuondoka kwa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli ni pigo kwa taifa na dunia kiujumla.
Akizungumza Championi Jumamosi, Saleh Nyenzi, Mjumbe wa Kamati
ya Utendaji alisema kuwa kutokana na msiba huo hawataweza kucheza mechi ya aina
yoyote huku wakiendelea kumuombea kiongozi huyo.
“Kwa kweli ni pigo kwa taifa na kwa sasa ni huzuni ambayo
imetawala kwani alikuwa ni moja ya viongozi wa mfano katika kutimiza majukumu
yake na alikuwa ni mpenda michezo.
“Kwa wakati huu timu bado ipo kambini nasi pia tunamuombea
Magufuli apumzike kwa amani, tunawaomba Watanzania wazidi kumuezi kwa mema
aliyofanya,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment