TANZIA
RAIS wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefariki dunia.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Samia Suluhu ametangaza msiba wa Rais, John Pombe Magufuli.
Samia usiku wa kuamkia leo kupitia television ya Taifa ya Tanzania, TBC amesema kuwa umauti umemkuta Magufuli alipokuwa akipatiwa matibabu.
Ameongeza kwa kusema kuwa Magufuli ametangulia mbele za haki kutokana na tatizo la moyo alilokuwa nalo muda mrefu.
Utaratibu wa kumpumzisha Magufuli utatolewa na Serikali ambapo kutakuwa na maombolezo ya siku 14 na bendera zitakuwa nusu mlingoti.
Magufuli atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwa Tanzania na jitihada zake katika kila sekta ikiwa ni pamoja na michezo.
Pumzika kwa Amani








Tutazidi kumkumbuka raisi wetu alichokifanya pia, alikua na mchango mkubwa kwa watanzania mungu amlaze mahara pema peponi na apumzike kwa amani (AMINA)
ReplyDeleteR I P
ReplyDeleteMbuyu umeanguka....RIP mtetezi wa wanyonge na taifa kwa ujumla.....tutakukumbuka daima katika harakati zako za kulikomboa taifa la tanzania kutoka katika umaskini ambazo kwa bahati mbaya mungu amekuchukua ukiwa bado hujazikamilisha.
ReplyDeleteMungu amlaze mahali pema peponi Aliweza kutusaidia wengi Mbele yako nyuma yetu
ReplyDeleteR.I.P Hayati magufuri tulikupenda ila mungu kakupenda zaidi
ReplyDelete