March 26, 2021

 


KLABU mbili za Afrika kutoka Misri zimeingia anga za kuwania saini ya nyota wa Simba, Luis Miquissone ili kupata saini yake.

Waarabu hao wa Misri ni Pyramids na Al Ahly ambazo zinataja kufuatilia kwa karibu mwendo wa nyota huyo mwenye mabao mawili kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kocha wa Al Ahly, Pitso Mosimane aliwahi kufanya kazi na Luis na aliweka wazi kwamba miongoni mwa wachezaji ambao walimpa tabu alipokutana nao Uwanja wa Mkapa alikuwa ni Luis.

"Luis ni mchezaji mzuri na anajua namna ya kufanya akiwa uwanjani hasa pale anapotafuta matokeo kwa ajili ya timu.

"Ninamtambua kwa sababu nimefanya naye kazi na anajua kukaa kwenye nafasi," .

Katibu Mkuu wa Simba, Arnold Kashembe amesema kuwa taarifa hizo bado hazijafika mezani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic