April 28, 2021

 




KOCHA Msaidizi wa Simba, Seleman Matola ameibuka na kutoa kauli ya kibabe kwa wapinzani wao kwamba watakachokifanya ni kutotoka katika nafasi ya kwanza waliyopo kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara hadi watwae ubingwa. 

 

Matola ameongeza kwamba kitu kikubwa ambacho wanachokifanya kwa sasa ni kupambana kwenye mechi zao kwa kushinda kwa ajili ya kufanikisha azimio lao la kutwaa ubingwa wa ligi kwa msimu huu.

 

 Kabla ya mechi ya jana, Simba wapo kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 58, moja mbele ya wapinzani wao Yanga ambao wana pointi 57.

 

 Matola ameliambia Championi Jumatano,kwamba kwa sasa plani yao ni kushinda mechi hizo ikiwemo zile za viporo kwa ajili ya kuendelea kukaa kileleni. 

 

“Mipango yetu kwa sasa ni kukaa kileleni na hatutashuka hadi tunachukua ubingwa wakati msimu ukiisha. 

 

Sisi tungekaa kwenye nafasi hii muda mrefu lakini mechi zetu za kimataifa zilikuwa zinatuchelewesha na kusababisha tuwe na viporo.

 

“Kwa sasa tutapambana tusitoke tena hadi mwisho wa msimu katika nafasi ambayo tupo na tutahakikisha mechi zetu zote ambazo ziko mbele tunashinda,” alimaliza

2 COMMENTS:

  1. Simba baba lao wapewe tu ubingwa wao maana wanastahili ubingwa kwa kiwango chao.

    ReplyDelete
  2. Jamani msienelee kuwatisha kwani tayari wameshakuwa watete na hswakijui wanachokifanys

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic