HEMED Morocco, Kocha Mkuu wa Namungo FC amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wao wa kesho wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Nkana FC ya Zambia na wanahitaji pointi tatu.
Namungo ipo
kundi D, imecheza mechi mbili na kupoteza zote, ilianza kupoteza mbele ya Raja
Casablanca bao 1-0 ugenini na ikapoteza kwa kufungwa mabao 2-0 dhidi ya
Pyramids, Uwanja wa Mkapa.
Inakutana na
Nkana FC ambayo nayo haijakusanya pointi baada ya kupoteza mechi zake zote
mbili kwenye makundi jambo ambalo litaongeza ugumu kwenye mchezo huo.
Akizungumza
na Saleh Jembe, Morocco amesema
alikusanya makosa kwenye mechi zilizopita jambo ambalo litawafanya
waingie uwanjani kwa namna nyingine.
“Makosa kwenye mechi zetu ambazo zimepita
yanatufanya tuingie kwa hesabu za tofauti kukutana na wapinzani wetu ambao
tunawaheshimu ila kwa kuwa tupo nyumbani hatuna mashaka.
“Wachezaji
wana morali kubwa na nimewaambia kwamba wanapaswa wajiamini kila kitu
kinawezekana. Ushindi ambao tutapata ni muhimu kwa timu na Tanzania kiujumla,”
amesema.
Dah wanazihitaji point tatu zao wenyewe
ReplyDeleteNamungo vs Namungo!! Hamko makini kabisa au ndo yale ya darasa la saba wanatosha!!
ReplyDeleteRekebisha heading
ReplyDeleteLabda Nkana ni ikiwa kwao Zambia lakini wakija bongo nao wanaitwa Namungo
ReplyDeleteAhahaha, kumbe Namungo FC ndio Nkana FC
ReplyDelete