BEKI wa kati wa Simba, Pascal Wawa raia wa Ivory Coast ameibuka na kutoa kauli ya vitisho kwa wapinzani wao Yanga katika Ligi kuu Bara kuwa, wasisahau kwa kujua Simba haina mpango na ubingwa kutokana na ushiriki wao katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Akizungumzia malengo yao, Wawa amesema kuwa kitendo cha wao kuwa bize na michuano ya kimataifa, isiwe sababu ya wapinzani wao wakiwemo Yanga, kuona urahisi kwa kuweza kutwaa ubingwa wa ligi kuu kwani hata wao bado wana malengo na kombe hilo.
“Unajua hii michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika ni migumu sana, lakini kadiri tunavyopiga hatua ndiyo matarajiao na malengo yetu yanazidi kuwa makubwa.
“Nadhani kuwa bize huku kusiwe sababu ya
wengine kusahau kuwa bado kuna mechi za
ligi, kwa sababu licha ya kushiriki ligi ya mabingwa bado tunahitaji kushinda
ubingwa wa ndani wa ligi hivyo haiwezi kuwa jambo rahisi,” amesema Wawa.
Sasa hivyo ni vitisho au kaongea mitazamo wake? Kweli mwandishi hujitambui.
ReplyDeleteNa sijui kama kweli amemhoji. Tumsamehe bure huyu mwandishi. Huenda anajifunza. Anatega vichwa vya habari vya kuvutia lakini ukisoma hakuna habar. Ni maelezo tu yasiyokuwa na kina. Kijana jiongeze. Mimi nimeanza kutokusoma vijihabari vyako maana naona kama unaviandika baada ya kuviwazia.
ReplyDelete