June 1, 2021

 


UONGOZI wa Yanga umesema kuwa bado una matumaini ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara uliopo mikononi mwa Simba.

Kwenye msimamo Yanga ipo nafasi ya pili ina pointi 61 huku watani zao wa jadi wakiwa nafasi ya kwanza na pointi zao 64.

Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amesema kuwa bado watazidi kupambana mpaka tone la mwisho kufikia malengo ambayo wameweka.

"Kikubwa ni kwamba tupo kwenye ushindani nasi tunapambana kupata matokeo mazuri, jambo la msingi ni kuona tunazidi kushirikiana na kuwa pamoja.

"Mashabiki waendelee kutupa sapoti ili kuona tunapata matokeo chanya, bado uwezo upo na nia ipo hivyo kazi inaendelea mpaka tone la mwisho," .

Simba inatetea taji hilo ambalo ilitwaa msimu uliopita na iliweza kutinga hatua ya robo fainali kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

2 COMMENTS:

  1. Mtaota sana Sana mpaja msinukiye kichwa chini na miguu juu na atayekufungen. Hakuna mwengine isipokuwa Morisson

    ReplyDelete
  2. Mimi ningependa Sana kumuona kumuona huyo Nguaz wakilpambana yeye na Manara kila mmoja akitowa yake tumuone mmja anavosanbaratika

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic